Psalms 60:1-6
Kuomba Kuokolewa
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Shushani Eduthi. Utenzi Wa Daudi. Wa Kufundisha. Wakati Alipopigana Na Waaramu Kutoka Aramu-Naharaimu Na Aramu-Soba, Yoabu Aliporudi Nyuma Na Kuwaua Waedomu 12,000 Katika Bonde La Chumvi)
1 aEe Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu,
umekasirika: sasa turejeshe upya!
2 Umetetemesha nchi na kuipasua;
uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
3 bUmewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa;
umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
4 cKwa wale wanaokucha wewe,
umewainulia bendera,
ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
5 dTuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,
ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
6 eMungu amenena kutoka patakatifu pake:
“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi
na kulipima Bonde la Sukothi.
Copyright information for
SwhKC